![]() |
MTUMISHI
WA MUNGU YESU ASIFIWE? (…)”ISAYA40: 27Kwa nini unasema, Ee Yakobo, nanyi Ee Israeli, kulalamika,“Njia
yangu imefichwa BWANA asiione,Mungu wangu hajali shauri langu?” 28Je wewe, hufahamu?Je wewe,
hujasikia?BWANA ni Mungu wa milele,Muumba wa miisho ya dunia. Hatachoka wala
kulegea,wala hakuna hata mmoja awezayekuupima ufahamu wake.”JIBU YEREMIA32; 27“Mimi ndimi BWANA, Mungu wa wote wenye
mwili, Je, kuna jambo lo lote lililo gumu nisiloliweza? NA ISAYA49;15 “Je,
mama aweza kumsahau mtoto aliyeko matitini mwake akinyonya?Wala asiwe na huruma
juu ya mototo aliyemzaa?Ingawa anaweza kusahau,Mimi sitakusahau wewe!
Namshuru MUNGU ambaye ametupa kusudi na sababu
angalau yakusema amina! Kwa sababu sio kwamba ni kwa juhudi au matendo ,lakini
neema ambapo tumestahilishwa kuwa tulivyo leo.Mtumishi (watumishi) wa MUNGU leo
nataka tuzungumzie dhana ambayo ni ya kawaida sana katika maisha ya kila siku
ya watu hasa wale ambao hawajui maana na
malengo ya damu ya yesu msalabani pale alipsema kuwa yote yamekwisha kwa dhamana
aliyoitoa kupitia aibu na mateso pale msalabani. Lakini lakushangaza na
kushutusha ni kwa wale watumishi wa MUNGU ambao wanatambua hayo yote ila bado
wanateteleshwa na kuhuzunishwa na hata mambo madogo ambapo baada ya kuwa
mabalozi na kuwatia moyo wale wanaokuwa katka ukristo na wale ambao wako nje
wanawakatisha tamaa na kuwavunja moyo kwa kuwaeleza kuwa hawatoweza hata kama
wameamua kusonga mbele na pia watu wakulalamika kila iitwayo leo hata kesho pia.LEO
tuzungumzie njinsi ya kuudhibitishia ulimwengu kuwa sisi ni wateule pia wana wa
Mungu na muda wote kuonekana mashujaa wa kristo wa ukweli.
1.
KUUMIZWA/KUUDHIWA AU
KUTESWA NA KUONEWA
Watumishi wa MUNGU pengine
tumekuwa watu wa kukata tamaa na pia watu wa kukata shauri za mapema sana hapa
bila kujali matokeo/madhara yatokanayo na maamuzi hayo kuenenda kwenye mashauri
ya kidunia na kusahau kuwa Mungu ni mkubwa zaidi ya hao tunaowakimbilia.
Mtumishi wa Mungu tusisahau kuwa huduma au utumishi ni vita vyenye mapambano
lakini utofauti vita hivi vin matokeo ya aina mbili tu tofauti vita vya dunia
ambavyo vina matokeo matatu ya ushindi,suluhu na kushindwa ; Vita vyetu ni
matokeo ya ushindi na kushindwa na si vinginevyo kwa hiyo na kwa mtumishi wa Mungu matokeo ni
ya aina moja tu pia kwa sababu ya mwanzilishi wetu ambaye naye anatwambia ‘SISI
NI WASHINDI SIKU ZOTE’a.UNAPOTESWA “ISAYA40; 29Huwapa nguvu waliolegea na huongeza nguvu
za wadhaifu.30Hata vijana
huchoka na kulegea,nao vijana wanaume kujikwaa na kuanguka,31bali wale wamtumainio BWANA atafanya
upya nguvu zao.Watapaa juu kwa mbawa kama tai,watapiga mbio wala
hawatachoka,watatembea kwa miguu wala hawatazimia.”b.
UNAPOONEWA
ISAYA14Kwa haki
utathibitika: kuonewa kutakuwa mbali nawe,hutaogopa cho chote.Hofu itakuwa
mbali nawe,haitakukaribia wewe.15Kama
mtu ye yote akikushambulia, haitakuwakwa ruhusa yangu,ye yote akushambuliaye
atajisalimisha kwako.CUMEVUNJIKA
MOYO”
ISAYA147:3Anawaponya waliovunjika mioyo
na kuvifunga vidonda vyao.
2. UMEATHRIKA KATIKA JAMBO FULANI AU TABIA
Watumishi wa Mungu
natamani leo tuongelee jambo dogo katika kutamka lakini ugonjwa ambao wa vizazi
au urithi ambayo kila mtu ukimpata ana dalili zake tofauti na mwingine ;Maana’ngu
ni hii hapa karibu kila mkristo au mtumishi wa MUNGU kuna dhambi
inamlazimisha kuitumikia miaka hadi
mingine hawezi kuishinda hadi imefika wakati anakiri hii ni dhambi yangu maana’ke
amekata tamaa na ameamua kuitumikia na kusahau kuwa dhambi ni uasi na
aifanyanye afanya uasi na pili kuwa atendaye dhambi ni wa shetani na pengine
anaweza hata kuitetea akijitafutia haki.Lakini neno la Mungu leo linatukumbusha
kuwa haitupasi kuitumikia dhambi bali kuikemea na kuichukia,kwasababu inabeba
mauti.Bado kuna nafasi na hakuna haja ya kukata tamaa ya kwenda mbinguni.”RUMI5 ;20Zaidi
ya hayo, sheria ilikuja, ili uvunjaji wa sheria uongezeke.”1YOHANA1 ;9Kama
tukiziungama dhambi zetu, Yeye ni mwaminifu na wa haki, atatusamehe dhambi zetu
na kutusafisha toka kwenye udhalimu wote. 10Kama tukisema hatukutenda dhambi, twamfanya Yeye kuwa mwongo na
Neno Lake halimo ndani yetu.na YOHANA 8; 36Hivyo
Mwana akiwaweka huru mtakuwa huru kweli kweli.
3.NDUGU/JAMAA/RAFIKI WA KARIBU
AMEATHRIKA KATIKA ARI AU JAMBO FULANI;
Watumishi wa mungu ebu
sasa tukumbushane na hili najua yawezekana ni wewe hata mimi tuna wapendwa wetu wameathriwa na mambo au hali mbalimbali
mfano madawa ya kulevya,sigara,pombe,madeni,uasherati na uzinzi ,lugha chafu na
hali nyinginezo hadi tumekata tamaa ya kuwa na ndugu tupendao wenye kunena
maneno ya busara. Lakini neno la Mungu leo lasema tusikate tamaa bado kuna njia
ya kutokea.Kupitia ushaidi huu.”1YOHANA5;14Huu ndio ujasiri tulio nao ndani Yake, kama
tukiomba kitu sawasawa na mapenzi Yake, atusikia. 15Nasi kama tunajua ya kuwa atusikia, lo lote tuombalo, tunajua ya
kwamba tumekwisha kupata zile haja tulizomwomba. .
4.UMERUDI NYUMA;
Watumishi wa MUNGU pia
wengine yawezekana tumekata tama kisa umeteleza kiroho hadi unapoona watumishi wenzako unahisi
kama wadeni wako ukimwona mchugaji unajificha. Hauna amani hadi umekata tamaa
au pengine umerudi nyuma kimaendeleo hadi umefikia kipindi unanena kama wasio
amini ,”maendeleo ni ya watu Fulani au Mungu ameniacha au amenisahau au
hanipendi .Lakini neno la Mungu linasema usikate tama.Hata kwa wanafunzi
yawezekana ufaulu umeshuka Mungu anasema bado kuna njia. “YEREMIA3; 22“Rudini,
enyi watu msio waaminifu, nami nitawaponya ukengeufu wenu.“Naam, tutakujia kwa
maana wewe ni BWANA, Mungu wetu.” EBRANIA8; 12Kwa kuwa nitasamehe
uovu wao,wala sitazikumbuka dhambi zao tena!”1YOHANA1; 9Kama
tukiziungama dhambi zetu, Yeye ni mwaminifu na wa haki, atatusamehe dhambi zetu
na kutusafisha toka kwenye udhalimu wote.
5.MATATIZO KAZINI
Kila mtu ulimwenguni nadhani anafurahi pale
anapofanya kazi yake katika mazingira ya utulivu ukizingatia kuwa
walio wengi kabla ya kupata kazi upita
mazingira magumu na muda mrefu ,kwa hiyo uhitaji kufanya kazi zao katika
hali ya utulivu wa wastani kama sio mazingira mazuri lakini tofauti na yalivyo
matarajio ya wengi mambo huwa tofauti ambapo wapo upata matatizo hata pengine
zaidi hata enzi kabla ya hizo kazi kwa hiyo watu uamua kuchukua maamuzi magumu
kama kwenda kwa wanganga wa kienyeji wakifta msaada na hata watumishi wa Mungu
wengine ukata tamaa ya kutegemaea Mungu nao njia za kidunia wakitafta msaada
lakini leo Mungu leo Mungu leo anasema nasi kuwa tusikate tama.Kupitia neno
lake;”ZABURI55;22Mtwike BWANA fadhaa zako,naye atakutegemeza,hatamwacha
kamwe mwenye haki wake aanguke”.1KORINTHO14; 33Kwa
Mungu si Mungu wa machafuko bali ni wa amani. Kama ilivyo katika makusanyiko
yote ya maana watakatifuWA,WARUMI 8; 28Nasi
tunajua ya kuwa katika mambo yote Mungu hutenda kazi pamoja na wote wampendao,
katika kuwapatia mema, yaani, wale walioitwa kwa kusudi Lake.PAMOJA ZABURI 55
18Huniokoa nikawa salama kutoka katika vita vilivyopangwa dhidi
yangu,ingawa watu wengi hunipinga.;
6.LAANA ZA VIZAZI(MABABU)
Tumekombolewa kwa damu ya mwana kondoo kwa
hiyo hakuna haja yoyote ya mtu Mungu kuongopa au kuendelea kuteswa na laana za
wazazi au mababu au ukoo vizazi na huku
Yesu Alisha twambia kuwa kwa
kupingwa kwake uponyaji wetu ulipatikana .Ndamu yake ilifuta kila laana
na mikosi kwa hiyo mtumishi wa Mungu hakuna sababu ya kuendelea kuteswa na
laana kama mfungwa aliyefutiwa makosa lakini bado yuko gerezani toka gerezani
kwa kumkumbusha maneno haya;GALATIA 3; 13Kristo
alitukomboa kutoka katika laana ya sheria kwa kufanyika laana kwa ajili yetu,
kwa maana imeandikwa, “Amelaaniwa yeye aangikwaye juu ya mti.”
7. MATATIZO YA NDOA
Watumishi wa MUNGU
naomba tuongelee jambo ambalo wengi wetu tunakata tamaa kwalo .Pale mwili ulioungnishwa
na kristo unapoonekana kuwa na nyufa watu tunaanza kufikilia unakwenda kubomoka
baada ya kufikili kuwa bado kuna tumaini la kuziba ! Na wengine tunafikilia
kuhama sehemu tukihisi uwezekano wa maisha kuendelea ni mgumu.Lakini leo MUNGU
anasema uwezekano wa kuendelea bado upo na pia kufika tuendako ni lazima. Kwa
hiyo hakuna sababu ya kuhuzunika au kukata tamaa . Licha ya njia au mapito
ambayo mwenzio anakupitisha ,fahamu kuwa ni kitambo tu ;bali una kusudi leo.ISAYA
32: 6Haki itakaa katika
jangwa na uadilifu utakaa katika shamba lenye rutuba. 17Matunda ya haki yatakuwa amani, matokeo ya haki yatakuwa utulivu
na matumaini milele. 18Watu
wangu wataishi katika makao ya mahali pa amani, katika nyumba zilizo salama,
katika mahali pa kupumzika pasipo na usumbufu. 19Ingawa mvua ya mawe iangushe msitu 20tazama jinsi utakavyobarikiwa, ukipanda mbegu yako katika kila
kijito, na kuwaacha ng’ombe wako na punda wajilishe kwa uhuru. YEREMIA32; 27“Mimi ndimi BWANA, Mungu wa wote
wenye mwili, Je, kuna jambo lo lote lililo gumu nisiloliweza?
LUKA 1:37Kwa
maana kwa Mungu hakuna lisilowezekana.”
8.WOGA/HOFU ( EBRANIA
13;6Kwa hiyo tunaweza kusema kwa ujasiri, Bwana ni msaada wangu,
sitaogopa, mwanadamu atanitenda nini?”)
Mungu
atusaidie watumishi ,natambua wazi kuwa yawezekana kwa hali ya kawaida hakuna
mtu ambayo hana hofu katika hali mbaya kwa katka ubinadamu lakini tukitambua
kuwa tuna ulinzi wa tofauti wa malaika wa Mungu ambao kila siku wako kazini kwa
ajiri yetu.Watumishi wa MUNGU nadhani tofauti na wafalme wa dunia ambao ulindwa
na binadamu wenzao ambao mda wowote waweza badilika lakini sisi ufaulme wetu ni
wa tofauti kwani MUNGU mwenyewe ndo jemadari katika kuwamuru malaika watulinde
sisi kwa hiyo hatuna haja wala sababu ya kuogopa hali au mazingira. 2TIMOTHEO1;” 7Maana
Mungu hakutupa roho ya woga, bali roho ya nguvu, ya upendo na ya moyo wa kiasi”.Watumishi pengine tunahofu na wenza wetu tumeshindwa
kuaamini ,wakitoka tu mioyo inakuwa juu lakini leo Mungu anasema upendo wa
kweli hauna wivu wala hofu.1YOHANA 4; 8Katika
upendo hakuna hofu. Lakini upendo ulio kamili huitupa nje hofu, kwa sababu hofu
inahusika na adhabu. Kila mwenye hofu hakukamilika katika upendo.
9.MATATIZO YA FAMILIA
Familia kwa
kawaida ni ile ambayo watoto ,baba na
mama na ndugu wengine wanaishi kwa upendo na furaha ikihusisha kusaidiana
lakini ,tofauti na matarajio familia nyingi hiyo hali imekuwa ya kusoma katika
vitabu vya historian a kwao wazazi wapo lakini ni yatima na wazazi wanakuwa
wajane na wagane wenza wao wakiwa bado hai .Ndugu kwa ndugu wanaishi visiwani
wakiwa hakuna usafiri wa majini au daraja
ili wakutane.Lakini leo mungu anasema bado kuna nafasi na njia kwa sababu,amejenga
daraja na kuvunja kuta kati yenu.ISAYA 32; 17Matunda
ya haki yatakuwa amani, matokeo ya haki yatakuwa utulivu na matumaini milele.18Watu
wangu wataishi katika makao ya mahali pa amani, katika nyumba zilizo
salama,katika mahali pa kupumzika pasipo na usumbufu.KUMB
26; 11Kisha wewe pamoja na Walawi na wageni wote walioko
miongoni mwenu mtafurahi katika vitu vyote vizuri ambavyo BWANA Mungu wenu
amewapa pamoja na wa nyumbani mwenu.ZAB127;1BWANA
asipoijenga nyumba, wajengao hufanya kazi bure.BWANA asipoulinda mji,walinzi
wakesha bure
10.UNAPOFIWA NA MPENDWA WAKO
Kiubinadamu huwa ni vigumu sana kutoonesha
huzuni ,kuweweseka ,kukosa kula,kukosa kuamini uakika wa kuwa salama kesho pale
tunapopoteza wapendwa wetu na mara nyingi ikitokea ni zaidi ya mara moja au
kupoteza wapendwa wengi kwa wakati mmoja pengine tunaweza kupingana na Mungu
katka maneno yake ktk ISA 49:15 na kusahau kushukuru hata kwa yale
aliyotusaidia katika mapito hayo. Lakini leo Mungu anasema bado lango la
matumaini liko wazi.MATAYO5;
4Wana heri wale wanaohuzunika,maana hao watafarijiwa.2KOR1; 3Ahimidiwe
Mungu na Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo, Baba wa huruma na Mungu wa faraja
yote. 4Yeye atufarijiye katika taabu zetu zote, ili tuweze kuwafariji
wale walio katika taabu yo yote kwa faraja ambayo sisi wenyewe tumepokea kutoka
kwa Mungu.ZABURI147; 3Anawaponya
waliovunjika mioyo na kuvifunga vidonda vyao.
11.GUVU ZA GIZA
Mpendwa nadhani sio mara
ya kwanza kusikia neno nguza giza au nguvu za mapepo ambapo baadhi ya watu
wanaendelea kuteseka kwa sababu ya nguvu hizo ,familia hakaliki kwa sababu ya
nguvu hizo. Pia wanafunzi wameachishwa shule kwa sababu hiyo ,hadi tumefikia
kipindi tumeamua kwenda kwa wachawi/waganga wa kienyeji kutafuta na kusahau
Mungu ambaye ndiye aliumba hata hao waganga. Lakini leo MUNGU leo anasema kuwa
bado kuna lango na hakuna haja kukata tamaa.LUKA10; 19Tazama
nimewapa mamlaka ya kukanyaga nyoka na ng’e na juu ya nguvu zote za adui, wala
hakuna kitu cho chote kitakachowadhuru kwa namna yo yote. YAKOBO4;7Basi
mtiini Mungu. Mpingeni Shetani, naye atawakimbia.YOHANA8; 36Hivyo
Mwana akiwaweka huru mtakuwa huru kweli kweli.
HITIMISHO
Watumishi wa Mungu mbarikiwe sana na malaika
wa Mungu wako zamu kuwalinda wala msiwe na hofu kwa sababu wanatimiza wajibu
wao ambao Mungu amwamuru kufanya .Pia mtumishi tumtumikie Mungu kwa uaminifu
naye hatatuacha bali ataendelea kututumia kwa kusudi lake kwasababu ni ahadi
yake kwamba atatimiza ahadi kuliko hat neno lake tusimsahau wala kusahau kazi
yake YEREMIA2; 32Je, mwanamwali husahau vitu vyake vilivyofanyizwa kwa
vito,bibi arusi husahau mapambo yake ya arusi? Lakini watu wangu wamenisahau
mimi,tena kwa siku zisizo na hesabu.